Anthonio


Breaking News

About

Become a Fan

Monday 21 July 2014

SHETTA AMWAGIWA UJI WA MOTO

KHA! Staa wa Kerewa, Nurdin Bilal ‘Shetta’ juzikati alijikuta katika wakati mgumu baada ya kumwagiwa uji wa moto na Mbongo-Fleva mwenzake, Mwajuma Abdul ‘Queen  Darleen’.
Staa wa Kerewa, Nurdin Bilal ‘Shetta’ akipewa dozi ya maji.
Tukio hilo la aina yake lilijiri muda mchache baada ya tafrija iliyoandaliwa na uongozi wa No Fake Zone ‘NFZ’ kwa ajili ya uzinduzi wa video mpya ya Linah na kuaga rasmi menejimenti ya Jumba la Vipaji Tanzania (THT) pande za Kinondoni jijini Dar.
‘Shetta’ aliyelowa chapa chapa.
“Unajua leo ni siku ya kuzaliwa ya Shetta, ikiisha tu hii shughuli namuita nje na kummwagia maji yeye mwenyewe anajua sisi hatujui,” alisikika Ommy Dimpoz.
Linah Sanga akizungumza jambo katika tafrija iliyoandaliwa na uongozi wa No Fake Zone ‘NFZ’ kwa ajili ya uzinduzi wa video yake mpya.
Baada ya tukio hilo ndipo Shetta alipotoka nje na kukutana na ishu hiyo ya kummwagia maji kisha Queen Darleen akamaliza mchezo kwa kummwagia uji.

No comments:

Post a Comment

Designed By